Thursday, March 30, 2017

JE UNAFAHAMU MADHUMUNI YA USAJILI WA VYOMBO VYA MOTO?
Kwa watu wengi, uelewa wao juu
ya madhumuni ya usajili wa vyombo vya moto unaishia kwenye kukusanya mapato.
Ukweli ni kwamba, pamoja na hilo kuwa ni moja kati ya madhumuni ya usajili wa
vyombo vya moto, bado kuna madhumuni mengine mengi ya usajili wa vyombo vya
moto kama vile; kuonesha uhalali wa umiliki wa chombo husika, ndio maana kadi
ya umiliki wa chombo husika hutolewa baada ya usajili.
Lakini pia usajili wa vyombo vya moto una dhumuni la kuonesha matumizi ya chombo
kilichosajiliwa kwa maana kwamba kama chombo kimesajiliwa kwa matumizi
*binafsi* ama kwa matumizi ya *biashara.*
Zaidi
ya hayo usajili wa vyombo vya moto unadhumuni la kuonesha aina ya chombo, kama
ni gari na ni gari la aina gani, ama ni pikipiki, trela, trekta mtambo,
nakadhalika.
Dhumuni
jingine la usajili wa vyombo vya moto ni kurahisisha uchunguzi wa uhalifu
endapo utafanywa kuhusisha chombo cha moto. Lakini pia usajili wa vyombo vya
moto hurahisisha utoaji wa taarifa mbalimbali zinazohusu vyombo vya moto kwa
taasisi nyingine. (Information/Statistical data), mfano ajali za kugonga na
kukimbia (Hit & Run accidents).
*Ndio
maana Kifungu cha 8 (i) cha Sheria ya Usalama barabarani namba 30/1973 (CAP 168
RE.2002)* inaeleza kuwa hairuhusiwi kwa mtu yeyote *kuendesha chombo cha moto
ambacho hakijasajiliwa.* Kipengele (2) cha sura hiyo hiyo kinaeleza adhabu kwa
mtu atakayekamatwa akitumia chombo cha moto ambacho hakijasajiliwa kuwa ni pamoja
na faini isiyozidi elfu hamsini za kitanzania au kifungo kisichozidi miaka
mitano.
ANGALIZO HAPA NI KWAMBA: *Kumekuwa
na taarifa za mitaani kuwa unaruhusiwa kutumia chombo cha moto kisichosajiliwa
mpaka saa 12 jioni na siku za mwisho wa wiki na sikukuu.* Taarifa hizo sio
sahihi, sheria inasema kwamba *hairuhusiwi kwa mtu yeyote kutumia chombo cha
moto ambacho hakijasajiliwa.
Hapa juu nimetaja sheria ya
usalama barabarani, Sheria ya Usalama Barabarani namba 30/1973 (CAP 168
RE.2002). Lakini si sheria hiyo pekee inayosimamia usajili wa vyombo vya moto. Kuna
sheria nyingine kama vile, Sheria ya Usajili na Ubadilishaji wa Umiliki wa gari
ya mwaka 1972. (Motor Vehicles Tax on Registration and Transfer Act of 1972).
*Hivyo kununua chombo cha moto chenye usajili wa mtu mwingine na kukitumia bila
kubadilisha umiliki ni kosa kisheria.* Hata hivyo kosa hili linaonekana ni la
kawaida sana kwa jamii hasa kutokana na ugumu wa maisha na watu wengi kushindwa
kununua magari mapya na hivyo kulazimisha kununua magari mikononi mwa watu
wengine yakiwa tayari yalisajiliwa kwa matumizi yao.
*Sheria inamtaka kila mmoja
kubadili umiliki mara baada ya kununua.*
Pia kuna kanuni mbalimbali za
usalama barabarani zilizoundwa chini ya sheria ya usalama barabarani ya mwaka
1973 kama ilivyorekebishwa mwaka 2002.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
JE UNALIFAHAMU GARI AINA YA AJBAN 440A?
Older Article
Girls must be protected against FGM
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment