Aliyekuwa Mume wa zamani wa Muigizaji Irene Uwoya na Mchezaji wa Burundi, Hamadi Ndikumana Katauti (39) amefariki dunia.
Taarifa za kifo cha Ndikumana zimethibitishwa na Muigizaji Irene Uwoya.
Ndikumana na Uwoya walifunga ndoa Julai 2009 na walifanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume ‘Krish’ na kisha baadae kutengana.
Mpaka anakutwa na mauti alikuwa akicheza katika timu ya APOP Kinyras Peyias FC ya Cyprus.
Hivi karibuni Irene Uwoya aliolewa na msanii wa Rap Tanzania Dogo Janja.

No comments:
Post a Comment