Friday, April 27, 2018

Benki ya Exim yapata faida ya Bilioni 9.6 kwa mwaka 2017
Benki ya Exim Tanzania imetangaza kupata faida ya bilioni 9.6 kwa mwaka 2017, faida ambayo imewawezesha kuwa benki ya tano nchini.
Akizungumza na wanahabari kuhusu faida ambayo benki hiyo imeipata, Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki ya Exim, Seleman Ponda alisema faida ya mwaka jana imekuwa kidogo kulinganisha na mwaka 2016 ambapo ilipata faida ya bilioni 83.6 kwa sababu mbalimbali ikiwepo kuongeza mikopo ambayo haijafanya.
“Benki yetu imekuwa ya tano nchini ikiwa na rasirimali za trilioni 1.6. Kwa mtaji wa benki umeendelea kuimarika zaidi, hadi Desemba 2017 tulikuwa na Bilioni 231 kwahiyo tunao uwezo wa kukabiliana na majanga ambayo yanaweza kutokea,” alisema Ponda.
Aidha alisema kwa sasa benki imejipanga kuboresha huduma zaidi kwa njia ya mtandao kwani ni njia rahisi kuwafikia wateja wengi, kwa urahisi na kwa gharama ndogo zaidi tofauti na inavyotumika sasa.
“Huduma za digitali ndio lengo letu, kuna huduma nyingi tunafanya kwa mtandao, kwa digitali tunafikia wateja wengi zaidi na kupunguza gharama za uendeshaji. Kwa mwaka 2018 na kuendelea tumepanga kuboresha huduma kwa mtandao,” alisema
Pia alizungumza uwajibikaji kwa jamii (CSR), “Mwaka uliopita lengo ilikuwa kutoa vitanda na magodoro kwa hospitali mbalimbali nchini kama sehemu na kusaidia jamii. Sekta ya afya ni muhimu na kila mtu anahitaji kuwa na afya bora hivyo tuliona tusaidie huko.”
Tags
# BIASHARA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
YALIYOJIRI MAGAZETINI LEO JUMAMOSI TAREHE 28, APRIL 2018
Older Article
Zoezi la kuwasikiliza wakinamama Waliotelekezwa lafanikisha Watoto 2008 kupata uhakika wa Matunzo kutoka kwa Baba zao.
Absa Group Reports 10% Increase in 2024 Earnings after Material Second-Half Recovery
Hassani MakeroMar 11, 2025Benki ya NBC Yaandaa Hafla ya Futari Zanzibar, Yajivunia Ongezeko la Wateja
Hassani MakeroMar 07, 2025BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA RASHAL ENERGIES, INAYOJENGA BOMBA LA GESI KISEMVULE-MBAGALA
Hassani MakeroMar 07, 2025
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment