Monday, February 18, 2019

Mwanamfalme wa Saudia akanusha madai ya kuinunua Manchester United
Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed Bin Salman amekanusha madai kuwa anantaka kuinunua Manchester United kwa kitita cha pauni bilioni 3.8.
Tetesi ziliibuka mwishoni mwa wiki zikimuhusisha mwanamfalme huyo na kutaka kuinunua klabu hiyo tajiri nchini Uingereza.
Wamiliki wa klabu hiyo, familia ya Glazers wanadaiwa kuwa hawana mpango wa kuiuza timu yao.
Wamiliki hao kutoka Marekani waliinunua Man United kwa kitita cha pauni milioni 790 mwezi Mei 2005.
"Ripoti zinazomuhusisha Mwana Mfalme Mohammed Bin Salman kuwa anataka kuinunua Manchester United ni uongo mtupu," amesema waziri wa michezo wa Saudia Turki al-Shabanah.
"Manchester United walifanya mkutano na mfuko wa uwekezaji wa umma PIF wa Saudia kuhusu nafasi ya udhamini. Lakini hakuna makubaliano yaliyofikiwa mpaka sasa," ameeleza waziri huyo.
Salman, 33, aliteuliwa kuwa mrithi wa kiti cha Ufalme wa Saudia Juni 2017.
Chini ya utawala wake, taifa hilo limelaaniwa vikali kwa visa vya kukiuka haki za binaadamu na kushutumiwa kwa mauaji ya mwanahabari Jamal Khashoggi katika ubalozi wa Saudia nchini uturuki mwaka jana.
Mwezi Oktoba mwaka jana, Manchester United ilijitoa kwenye mazungumzo na PIF baada ya mauaji ya Khashoggi.
Tags
# MICHEZO
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
Serikali haitamvumilia atakayebainika kuhujumu mkakati huu
Older Article
Uber yazindua bima ya Ulinzi dhidi ya Majeraha kwa madereva na abiria nchini Tanzania bila gharama yoyote ya ziada
TAARIFA KUTOKA BODI YA LIGI KUU TANZANIA
Hassani MakeroMar 08, 2025WAKAZI WA DAR WAJITOKEZA KUCHUKUA NAMBA KUSHIRIKI MBIO ZA YAS KILI INTANATION HALF MARATHON
kilole mzeeFeb 15, 2025KOCHA WA YANGA APEWA MKONO WA KWAHERI
Hassani MakeroFeb 04, 2025
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment