BASI LA PREZEDAR LAPINDUKA KITONGA LAUA 10 NA KUJERUHIWA 50 - Wor'Out Media

Wor'Out Media is a premier site for selected informative articles from Tanzania, East Africa and the rest of the world. We operate 24 hours a day, 365 days a year with complete context, perspective and precision.

Breaking

Saturday, June 27, 2020

BASI LA PREZEDAR LAPINDUKA KITONGA LAUA 10 NA KUJERUHIWA 50






Abiria 10 wamepoteza maisha na 50 wejeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Prezedar lililokuwa likielekea  Dar es Salaam kutumbukia korongoni baada ya break kufeli 

Mganga mfawidhi wa Hospitali  teule ya Misheni Ilula Dkt Benjamin Chota ameeleza kuwa hadi majira ya saa 1:30 usiku walikuwa wamepokea maiti 4 na taarifa toka sehemu ya ajali kuwa kuna maiti 6  zipo njiani .

Kati ya maiti hizo vijana wanaosadikika kuwa na miaka 18 ni maiti mbili na watoto chini ya miaka mitano wawili ndizo maiti zilizofika.

Wakati majeruhi 50 watu wazima ni 33 Kati yao wanaume 16 wanawake 17 na watoto chini ya miaka 18 wapo 17 Kati yao wakike ni 7 wavulana 10 .

Utambuzi wa maiti bado unaendelea.

No comments:

Post a Comment

Sharing Buttons

Pages