Thursday, July 9, 2020

DK TULIA ACHANGIWA FEDHA ZA KUCHUKULIA FOMU YA UBUNGE NA VIONGOZI WA KIMILA
Umoja wa viongozi wa kimila (MACHIFU) pamoja na Wazee wa Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya leo wamefika nyumbani kwa Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson na kumpatia pesa taslim ambazo wamezichanga kwa umoja wao ili ziweze kumsaidia kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo ambalo anatarajia kugombea kwenye uchaguzi mkuu 2020 ambalo hadi sasa hajalitaja.
“Tumekuja kwa ajili ya kumtakia kila la kheri katika kule anakokwenda kugombea, sisi kama wazazi tumemkubalia na tunamtakia mafanikio mema huko anakotaka kwenda”
“Tunafahamu kwamba ametia nia ya kugombea nafasi ya Ubunge, kikubwa kilichotusukuma kufanya hiki leo ni kutokana na jitihada kubwa alizozifanya na anazozifanya katika taifa letu kwenye maeneo mbalimbali”- Joel Mwakatumbula, Mkuu wa Machifu Rungwe
Kwa upande wake Dkt. Tulia amesema "Niwashukuru sana Wazazi wangu hawa kwa upendo mkubwa walionionesha pamoja na Baraka zao, ni wazi pengine ningeweza kupungukiwa hiyo pesa lakini wakaona mtoto wetu asijekuacha kuchukua fomu kwa kukosa hiyo pesa. Hakika wameianzisha safari ambayo na wao wameona ulazima wa kuwa sehemu ya safari hiyo” –Dkt. Tulia.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
Watiania Ubunge Wa CCM Mkoa Wa Iringa Waonywa Kuzingatia Sheria Na Kanuni Za Chama
Older Article
VODACOM TANZANIA FOUNDATION YATOA ZAWADI KWA WASHINDI WA MASHINDANO YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA NA UBUNIFU (MAKISATU 2020)
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment