Thursday, July 2, 2020

GWAJIMA kugombea UBUNGE - KAWE kwa tiketi ya CCM!
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima, ametangaza nia ya kutaka kugombea ubunge katika jimbo la kawe.
Gwajima ametoa uamuzi huo jana kwamba atagombea kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo hilo.
Jimbo hilo ambalo linashikiliwa na aliyekuwa mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee.
Gwajima jana alifika katika ofisi za CCM Wilaya ya Kinondoni kwa ajili ya kuchukua fomu na kupokelewa na viongozi wa chama hicho.
“Mimi nilikwenda pale kama mimi kama mlivyomsikia mheshimiwa Rais na Dk Bashiru alivyosema wale watu wenye nia ya kumsaidia mheshimiwa Rais kuwatimizia wananchi adhima yao basi waanze kupitapita kwenye ofisi za chama na kuangalia nini kinawezekana,’ alisema Gwajima.
Aliongezea kuwa “Na mimi nikaanza kupita pita pale kuangalia na nimuombe na Mungu nione kama Mungu akiniruhusu nitaendelea. Nimefika pale nimemkuta Mwenyekiti na Katibu wakanipa maelekezo na miiko ya kufanya,” alisema Gwajima.
Alisema yeye anaishi Kawe “Nitagombea Kawe naona kunanoga pako vizuri,”
Juzi Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Ally Bashiru alitangaza wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali ruksa kuanza kujitokeza na kuchukua fomu.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
Zantel Yazindua Duka Jipya lililopo Vuga, Wazingatia Afya za Wateja Wao
Older Article
ECOBANK TRANSNATIONAL INCORPORATED HOLDS ITS 32ND AGM AND SHAREHOLDERS APPROVE RESOLUTIONS
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment