Thursday, July 2, 2020

Home
KITAIFA
NAIBU WAZIRI MAVUNDE AWASHUKIA WAAJIRI WASIOWASILISHA MICHANGO NSSF, ATOA MAAGIZO MAZITO
NAIBU WAZIRI MAVUNDE AWASHUKIA WAAJIRI WASIOWASILISHA MICHANGO NSSF, ATOA MAAGIZO MAZITO
Naibu Waziri wa Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde leo ameanza utekelezaji wa agizo la kuwachukulia hatua za kisheria waajiri wote wasiowasilisha michango ya wafanyakazi katika mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF.
Naibu Waziri Mavunde alitoa agizo tarehe 9.06.2020 la kuwataka waajiri wote ambao hawajawasilisha michango ya wafanyakazi katika mfuko wa NSSF kufanya hivyo ndani ya wiki mbili vinginevyo hatua kali dhidi yao kuchukuliwa.
"Kumkata Mfanyakazi michango ya NSSF kwenye mshahara na kutokuwasilisha michango katika mfuko kwa kubadili matumizi ya fedha hizo ni tendo la uwizi kama ulivyo uwizi mwingine wowote.
Nimetoa maagizo kwa Wanasheria wa NSSF kujadiliana na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka ya Umma kama makosa haya ya kukata fedha za wanachama na kuzitumia kwa malengo tofauti bila kuwasilisha kwenye mfuko husika haidondokei katika makosa ya Utakatishaji fedha"Alisema Mavunde.
Wakati huo huo Naibu Waziri Mavunde ameelekeza kukamatwa na kuhojiwa kwa wamiliki wa Kampuni ya D.B. Shapriya Co Ltd kutokana na kushindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi,na pia kumtaka Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Q Rent Tanzania Ltd ,kupitia mawasiliano ya simu,kufika saa 3:00 na nyaraka zote za malipo ya wafanyakazi katika ofisi ya Meneja wa NSSF na kutoa maelezo kwanini asichukuliwe hatua kwa kushindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
MAKAMU WA RAIS, SAMIA AENDELEA NA ZIARA YA KICHAMA MKOA WA MAGHARIBI UNGUJA
Older Article
NAIBU WAZIRI WA AFYA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA CCBRT
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment