Thursday, July 9, 2020

TAHA KUWAFUNDISHA WAJASILIAMALI WAO NJIA BORA ZA USINDIKAJI
Dar es Salaam.
Wakulima wanaojishughulisha na Mazao ya kilimo biashara ya Mbogamboga, Matunda na Viungo maarufu kama ‘Horticultural’ wameshauriwa kujiendeleza kwa kujifunza namna bora ya kuongeza thamani Mazao yao kwa njia ya usindikaji.
Akiongea katika ziara maalum ya mafunzo ya namna ya usindikaji na vifungashio vya bidhaa kwenye Maonyesho ya Biashara ya 44 Sabasaba kwenye Banda la TWCC, Mratibu wa Jinsia na Lishe wa Tasisi inayojishughulisha na Kilimo cha Mbogamboga,Matunda na Viungo Nchini (TAHA) Salome Stephen, amesema kuwa wakulima wa mazao hayo wanaweza kufanikiwa Zaidi katika swala zima la usindikaji wa Mazao yao.
Amesema kuwa Taasisi yao yenye Makao yake Makuu Jijini Arusha imeweza kuwapeleka Wanachama wao 20 kutoka Arusha, Pemba na Unguja kwa lengo la kuona na kujifunza kutoka kwa wajasiliamali wenzao walioko chini ya TWCC namna bora ya usindikaji wa Mazao na kutengeneza mtandao na mahusiano baina yao.
“tumekuja na Wajasiliamali 2o hapa, hawa ni wasindikaji ili kujifunza masuala ya usindikaji kutoka kwa wenzao na kutumia Vifaa vipya vya kufanya ‘Packaging’ na kujionea bidhaa mpya na Mashine Mbalimbali za Usindikaji” alisema Salome.
Aidha amesema kuwa TAHA ina lengo la kuendeleza tasnia ya ‘Horticultural’ Nchini kwa kujishughulisha na Mnyororo wa Mazao ya Mbogamboga, Matunda na Viungo ambapo wanawawezesha kwa kuwapa mafunzo ya Kiteecknolojia na mbinu bora za Kilimo Biashara.
“Sisi kama TAHA licha ya Masuala ya Mnyororo wa Mazao pia tunawapa wakulima wetu mbinu bora za Kilimo biashara na Tekinolojia ya kisasa ambapo inawasaidia kuweza kulima kilimo cha faida” alisema Salome.
Taasisi ya TAHA yenye Makao yake Makuu Jijini Arusha ina wanachama Zaidi ya elfu 40 nchi nzima katika mikoa 23 ya Bara na Visiwani.
Tags
# BIASHARA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
MATUKIO MBALIMBALI KATIKA BANDA LA TRA KWENYE MAONESHO YA SABASABA JIJINI DAR
Older Article
Watiania Ubunge Wa CCM Mkoa Wa Iringa Waonywa Kuzingatia Sheria Na Kanuni Za Chama
Absa Group Reports 10% Increase in 2024 Earnings after Material Second-Half Recovery
Hassani MakeroMar 11, 2025Benki ya NBC Yaandaa Hafla ya Futari Zanzibar, Yajivunia Ongezeko la Wateja
Hassani MakeroMar 07, 2025BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA RASHAL ENERGIES, INAYOJENGA BOMBA LA GESI KISEMVULE-MBAGALA
Hassani MakeroMar 07, 2025
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment