Saturday, November 6, 2021

BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO (TADB) YAAHIDI KUENDELEA KUINUA ZAO LA ZABIBU NCHINI
Na.Alex Sonna, Dodoma | Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) imeahidi kuendelea kuinua zao la zabibu nchini ili kuwezesha kuongeza uzalishaji na tija kwa wakulima.
Hayo yamesemwa na Meneja wa Kanda ya Kati wa Benki hiyo, Yodas Mwanakatwe wakati wa Tamasha la Mvinyo Dodoma maarufu kama Dodoma Wine Festivals.
Meneja huyo amesema kuwa TADB imewezesha wazalishaji wa zao la zabibu pamoja na wachakataji wa zao hilo.
“Tumeweza kutoa mikopo yenye zaidi ya thamani ya Tsh. Mil 700 na kunufaisha watu 186 waliopo katika mnyororo wa thamani wa zao la zabibu.” amesema Mwanakatwe
Kwa mipango ya mbeleni, Mwanakatwe ameeleza kuwa benki hiyo inajipanga pia ili kuweza kuwawezesha wakulima zaidi na waongezaji thamani wa zao la zabibu wakati na wakubwa ili kukabiliana na tatizo la upotevu wa zabibu baada ya kuvunwa.
Kwa upande wake mmoja wa wanufaika wa mikopo hiyo, Katibu wa Chama cha Ushirika Wakulima wa Zabibu na Masoko Mpunguzi (WAMAZAMA), Emmanuel Temba ameishukuru benki hiyo kwa mkopo uliowawezesha kuanza kuzalisha mvinyo.
“Awali tulipata changamoto ya kuweza kununua na kulipa kwa wakati wakulima wetu. Baada ya mkopo kutoka TADB, sasa tunalipa kwa wakati na wakulima wamepata uhakika wa soko la mazao yao wanapovuna."
Baada ya mkopo wa TADB, WAMAZAMA pia wameweza kununua mashine zinazotumika kuongeza thamani zao la zabibu kwa kutengeneza na kuhifadhi mchuzi wa zabibu (grape concentrate).
“Mchuzi huu wa zabibu tunawauzia wazalishaji wa mvinyo wakubwa. Hii imetusaidia kuongeza tija kwenye kilimo cha zabibu. Wakulima wetu sasa wanapata kipato zaidi,” ameeleza Katibu huyo.
Tanzania inauwezo wa kuzalisha tani 150,000 ya zabibu na kwa sasa inazalisha wastani wa tani 16,000 tu. Hii inatoa fursa kwa vijana na wadau wengine kuwekeza katika sekta hii.
Tags
# BIASHARA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
Shangwe za uzinduzi wa Absa Tanzania Health Club
Older Article
AIRTEL NA PRECISIONAIR WASHUSHA BEI TIKETI KWA WANAOLIPIA KUPITIA AIRTEL MONEY
Absa Group Reports 10% Increase in 2024 Earnings after Material Second-Half Recovery
Hassani MakeroMar 11, 2025Benki ya NBC Yaandaa Hafla ya Futari Zanzibar, Yajivunia Ongezeko la Wateja
Hassani MakeroMar 07, 2025BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA RASHAL ENERGIES, INAYOJENGA BOMBA LA GESI KISEMVULE-MBAGALA
Hassani MakeroMar 07, 2025
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment