Monday, November 8, 2021

Home
BIASHARA
TARATIBU ZA URASIMISHAJI WA BIASHARA KWA KUSAJILI NA KUTOA LESENI ZA BIASHARA NA VIWANDA KWA NJIA YA MTANDAO KUPITIA BRELA ZIMESAIDIA KUVUTIA WAWEKEZAJI: MHE. KIGAHE
TARATIBU ZA URASIMISHAJI WA BIASHARA KWA KUSAJILI NA KUTOA LESENI ZA BIASHARA NA VIWANDA KWA NJIA YA MTANDAO KUPITIA BRELA ZIMESAIDIA KUVUTIA WAWEKEZAJI: MHE. KIGAHE
NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe ameeleza kuwa taratibu za urasimishaji wa biashara nchini kwa kusajili na kutoa Leseni za biashara na viwanda kwa njia ya mtandao kupitia BRELA zimesaidia kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi na kuwezesha nchi kuwa katika kiwango bora cha ufanyaji biashara duniani.
Mhe. Kigahe ameeleza hayo Novemba 08, 2021 katika kikao cha mafunzo kwa Wabunge wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania kuhusu makapuni na majina ya biashara; leseni za biashara na za viwanda; na miliki ya ubunifu yaliyotolewa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma.
Mhe. Kigahe amebainisha kuwa utoaji huduma za BRELA kwa njia ya mtandao umepunguza sana na kudhibiti vishoka waliowasumbua wateja wakati walipohitaji huduma kama kusajili makampuni na majina ya biashara.
Aidha, Mhe. Kigahe ameeleza kuwa kupitia utekeleza wa Blueprint watapitia baadhi ada na tozo zinazotozwa na BRELA kwa kuziondoa au kuzipunguza ili Watanzania waweze kurasimisha biashara zao vilevile baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikiwakumba wateja kwenye mtandao zimetatuliwa na wanaendelea kufanyia maboresho Zaidi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Leseni BRELA, Bw. Andrew Mkapa wakati akitoa mafunzo juu ya usajili wa makampuni na majina ya biashara amefafanua kuwa baadhi ya wateja wamekuwa wakishidwa kutofautisha kati ya kampuni na jina la biashara huku akieleza kisheria ni vitu viwili tofauti.
Tags
# BIASHARA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
BODI YA NAFAKA NA MAZAO MCHANGANYIKO (CPB) KUUZA NAFAKA NCHINI KENYA
Older Article
ELIMU YA FEDHA KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI
Absa Group Reports 10% Increase in 2024 Earnings after Material Second-Half Recovery
Hassani MakeroMar 11, 2025Benki ya NBC Yaandaa Hafla ya Futari Zanzibar, Yajivunia Ongezeko la Wateja
Hassani MakeroMar 07, 2025BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA RASHAL ENERGIES, INAYOJENGA BOMBA LA GESI KISEMVULE-MBAGALA
Hassani MakeroMar 07, 2025
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment