Friday, May 19, 2017

OPERESHENI YA DOREEN YAFANIKIWA MAREKANI
Habari kutoka Hospitali zinasema Mtoto Doreen
amemaliza salama kufanyiwa upasuaji wa UTI wa MGONGO, kwa kile ambacho
madaktari wamesema kumefanikiwa kwa ufanisi mkubwa kupita matarajio yao.
Mtoto Doreen alikuwa afanyiwe upasuaji kwa
makadrio ya masaa 5:30, lakini zoezi hilo lilikamilika kwa muda wa masaa 4:00,
huku TEAM ya "Surgical Support" ikiwa na watu 6, na kwa pamoja
wakiongozwa na madaktari bingwa 2, Dr. Meyer na Dr. Durward. Doreen amehamishwa
kutoka chumba cha upasuaji na kupelekewa ICU, na madaktari wamesema kwa kuwa
hali yake imeridhisha sana, baadaye leo watamtoa ICU na kumrudisha wodi ya
watoto ambako ataendelea na mapumziko.
MUNGU amesikia MAOMBI ya watanzania na wote
waliotoa SALA na DUA zao kwa ajili ya mtoto Doreen popote Duniani.
Mtoto Wilson kwa mara kwanza ametoka nje ya
Jengo Kuu la Hospital ya Mercy akiwa kwenye "wheelchair", huku Mama
na Daktari wake wakiwa na tabasamu.
Mtoto Sadia akiwa na Dkt. Steve Joyce, ambaye
ni Daktari wake wa "Internal Medicine". Madaktari wanasema Binti
Sadia ni MUUJIZA wa Mungu kutokana na HALI aliyokuwa nayo kabla ya huduma ya
UPASUAJI. Asanteni SANA kwa DUA na SALA zenu.
Tags
# KIMATAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
R.I.P Reema Lagoo
Older Article
'UNTOLD STORI' YAWA GUMZO MAKUMBUSHO YA TAIFA DAR ES SALAAM
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ashiriki Mkutano wa Kamati ya Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi
Hassani MakeroFeb 16, 2025RAIS SAMIA AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA MSUMBIJI
Hassani MakeroFeb 15, 2025A Tanzania doctor receives International Award
kilole mzeeJan 15, 2025
Labels:
KIMATAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment