Saturday, February 3, 2018

DIWANI MDOE AANZA KUTATUA KERO ZA WANANCHI WA KATA SALANGA
Diwani wa kata ya Salanga jijini Dar es salaam Harun Mdoe amekuwa na mpango mkakati wa mda mfupi na mrefu kuhusiana na barabara ambayo kwa sasa imekua kero kwa wananchi wa eneo hilo.
Mdoe amesema hayo leo alipotembelea barabara hiyo ambayo inaunganisha Matangini, Michungwani, King'ongo, Matosa, Kata ya Goba pia kuelekea Bagamoyo ambapo kwa mkakati wa mda mfupi wamekuwa wakiweka vifusi ambavyo vinasaidia angalau kupitika kwa urahisi.
Kutokana na kero hiyo pia amewataka wananchi wanaoishi maeneo hayo kuacha mara moja tabia ya kumwaga maji barabarani ambayo yanasababisha uharibifu na wataoendelea kufanya hivyo watachukuliwa hatua za sheria.
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Michungwani Ismaili Kipungula amesema kuwa kuna shida kubwa katika barabara hiyo ambayo inaunganisha mitaa mitatu.
"hii barabara imekuwa ni tatizo kwamba imeoza na sio kuharibika tumejaribu kuhangaika kama mtaa tukishirikiana na wananchi pamoja Diwani wetu kama mnavyoona hizi ni jitihada za wananchi wenyewe lakini barabara bado sio nzuri hivyo tunaiomba Serikali waiangalie hii barabara pia wenzetu wa Tarura ambao wamekubali kutengeza wafanya haraka kwani ilifika hatua tulika mawasiliano" amesema Kipungula
Aidha kwa upanda wake mkazi na mtumiaji wa barabara hiyo Upendo Mbise amesema kuwa kina mama wamekuwa wakijifungulia njiani kutokana na adha na ubovu ulipo mimi mwenyewe nikiwa kama shahidi juzi mama mmoja alijifungulia njiani hali ambayo ni hatari pia inaweza kupelekea hata kifo
Tags
# KITAIFA
Share This
About kilole mzee
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Uchambuzi wa bajeti kuchochea ufanisi taasisi za umma
Hassani MakeroMar 24, 2025KAMPENI YA 'NO REFORM NO ELECTION' YAPOTEZA MWELEKEO RUKWA
Hassani MakeroMar 24, 2025TAMASHA LA KUOMBEA UCHAGUZI KUFANYIKA MIKOA YOTE TANZANIA
Hassani MakeroMar 24, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment