Tuesday, September 17, 2019

Home
KITAIFA
RC MAKONDA Atimiza Ahadi ya Kuwalipia Ada ya Kidato Cha Tano na Sita kwa Watoto wa Kike 100 Kutoka Familia Duni Waliofaulu Masomo ya Sayansi na Kushindwa kuendelea na Masomo kwa kukosa Ada.
RC MAKONDA Atimiza Ahadi ya Kuwalipia Ada ya Kidato Cha Tano na Sita kwa Watoto wa Kike 100 Kutoka Familia Duni Waliofaulu Masomo ya Sayansi na Kushindwa kuendelea na Masomo kwa kukosa Ada.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda
akimkabidhi bahasha yenye hundi ya malipo ya Ada ya shule na matumizi ya msingi
kwaajili ya masomo yake, kwa mmoja wa wanafunzi aliyenufaika ufadhili huo,
(kulia) Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE Bw. Khalfan Abdulrahman
Al-Mazouqi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiwa
katika picha ya pamoja na wanafunzi wanufaika wa ufadhili wa kulipiwa Ada ya
Kidato Cha Tano na Sita kwa Watoto wa Kike 100 Kutoka Familia Duni Waliofaulu
Masomo ya Sayansi na Kushindwa kuendelea na Masomo kwa kukosa Ada.
Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE Bw. Khalfan Abdulrahman Al-Mazouqi akimkabidhi bahasha yenye hundi ya malipo ya Ada ya shule na matumizi ya msingi kwaajili ya masomo yake, kwa mmoja wa wanafunzi aliyenufaika ufadhili huo.
Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE Bw. Khalfan Abdulrahman Al-Mazouqi akimkabidhi bahasha yenye hundi ya malipo ya Ada ya shule na matumizi ya msingi kwaajili ya masomo yake, kwa mmoja wa mzazizi wa mwanafunzi aliyenufaika ufadhili huo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wanufaika wa ufadhili wa kulipiwa Ada ya Kidato Cha Tano na Sita kwa Watoto wa Kike 100 Kutoka Familia Duni Waliofaulu Masomo ya Sayansi na Kushindwa kuendelea na Masomo kwa kukosa Ada.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul
Makonda September 17 ametimiza ahadi ya ufadhili wa Masomo kuanzia Kidato cha
Tano hadi Sita kwa Watoto wa kike 100 kutoka familia duni waliofaulu masomo ya
Sayansi lakini wakashindwa kuendelea na masomo kwa kukosa Ada ambapo katika
ufadhili huo amewalipia Ada na Vifaa ya shule ikiwemo Sare, mabegi, vitabu,
madaftari na Nauli.
RC Makonda amesema lengo la ufadhili huo ni
kumkomboa mtoto wa Kike kutoka familia duni aweze kupata elimu bora
itakayosaidia kubadili maisha ya Familia na mwisho wa siku kuwa na Taifa lenye
Wanawake Wanasayansi na Wagunduzi.
Aidha RC Makonda amesema ufadhili huo unaenda
sambamba pia na kumuunga Mkono Rais Dkt.John Magufuli alieamua kumkomboa mtoto
wa mnyonge kwa kutoa elimu bure kuanzia Darasa la Kwanza hadi kidato cha nne na
yeye ameamua kupokea kijiti kwa kuwasomesha kidato cha tano na Sita ili
wakifika vyuo vikuu wanufaike na Mkopo.
Hata hivyo RC Makonda amesema zoezi hilo
litakuwa endelevu kila mwaka ambapo amewahimiza wanafunzi waliobahatika kupata
fursa hiyo waitumie vizuri huku akimshukuru Balozi kwa Kumuunga mkono katika
kampeni hiyo.
Kwa upande wake Balozi wa Umoja wa Falme za
Kiarabu UAE Bw. Khalfan Abdulrahman Al-Mazouqi amesema ufadhili huo ni
Mwendelezo wa Kuunga Mkono juhudi za RC Makonda kwenye kila jambo kwakuwa
amekuwa mtu wa kupigania maslahi ya Wananchi anaowaongoza.
Tags
# KITAIFA
Share This
About Hassani Makero
Hassani Makero is a Wor'Out Media Country Manager located at Unguja-Zanzibar, Tanzania performing all technical issues concerning of Media Broadcasting activities, Satellites, and FM and Television equipments supplier.
Aside from that, Hassani Makero is also a Writer, Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 10 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs.
Aside from all above he own and operate his Blog known as Wor’Out Media since 2014.
Newer Article
WAZIRI MKUU AAGIZA GARI LA WAGONJWA LIPELEKWE IFAKARA
Older Article
WAZIRI MKUU AWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI SABA
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAKOREMO-MGONGORO
Hassani MakeroMar 12, 2025"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank
Hassani MakeroMar 12, 2025HALMASHAURI KUU YA CCM YAPENDEKEZA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA UTEUZI WA WAGOMBEA UONGOZI
Hassani MakeroMar 11, 2025
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment